MARUDIO_KISWAHILI-KIDATO CHA KWANZA_01

 


MARUDIO _KISWAHILI_KIDATO CHA KWANZA-01

1.Eleza maana ya maneno yafuatayo;

(a)lugha-ni sauti za nasibu zenye kubeba maana zinazotumika na jamii fulani kwa kusudi la mawasiliano.

     >nasibu-hakuna mahusiano ya moja kwa moja ya neno na kitu.

(b)Fasihi-ni sanaa itumiayo lugha kufikisha ujumbe katika jamii iliyokusudiwa au husika.

(c)Sarufi- ni mfumo wa kanuni za lugha zinazomuwezesha mzungumzaji kutunga sentensi sahihi na zenye kukubalika na wazawa.

(d)Kamusi-ni kitabu cha marejeo chenye orodha ndefu ya misamiati ya lugha Fulani na misamiati hiyo imefafanuliwa kwa kueleza maana zote zinanazokubalika kwa watumiaji wa lugha .

(e)Nomino-ni neno linalotaja vitu ,viumbe,hali au tendo ili kuviainisha na kuvitofautisha/kuvipambanua miongoni mwa vitu vingine.

#FOR HOMETEACHING SERVICE  CALL/SMS  0622813263

No comments

Powered by Blogger.